TMA YATOA TAHADHARI, SIKU TATU ZA MVUA MIKOA IFUATAYO

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam. 

Dar es Salaam. Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari siku tatu, kuhusu uwezekeno wa mvua kubwa zitzkazoweka kusababisha mafuriko, katika baadhi ya mikoa ya Pwani ikiwemo Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na TMA leo Jumanne Aprili 07, 2026 imesema mvua hizo zinatarajia kuanza Jumatano hadi Ijumaa, zikihusisha mikoa ya Lindi, Mtwara, Tanga, Pwani, Dar es Salaam sambamba na visiwa vya Unguja na Pemba.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa, uwezekeno wa kunyesha kwa mvua hizo pamoja na athari zake umeainishwa kuwa wa kiwango cha kati, lakini wananchi wametakiwa kuchukua tahadhari zote muhimu.

“Kuanzia kesho hadi Ijumaa mvua zinatarajiwa kunyesha katika maeneo tajwa, uwezekeno wa athari zake zipo katika kiwango cha kati” Imeeleza sehemu ya taarifa hiyo.

Hata hivyo TMA imeonya kuwa, mvua hizo zinaweza kusababisha mafuriko katika baadhi ya maeneo na kuathiri katika shughuli za kijamii na kiuchumi.

Wananchi wanaoishi katika maeneo ya Pwani na visiwani, wametakiwa kuwa waangalifu zaidi kutokana na uwezekano wa ongezeko la kiwango cha mvua.

“Umma unashauriwa kufuatilia taarifa rasmi za hali ya hewa na kuchukua tahadhari stahiki” Imeongeza taarifa hiyo.

TMA imeongeza itaendelea kufuatilia mwenendo wa hali ya hewa na kutoa taarifa zaidi kadri itakavyo hitajika.

Chapisha Maoni

0 Maoni